Huduma ya Kiroho

kuwa karibu na wewe

Kuianza siku

Tunaanza na adhimisho la Misa takatifu (Kanuni ya Kirumi) kila siku asubuhi

Kuwa karibu

Mapadre wamisionari, masista na makatekista wanatoa huduma ya kuwasaidia, kuwasikiliza na kuwafariji wagonjwa.

Hospitali ya kila mtu

Kwa mahitaji, viongozi wa imani zingine hutoa huduma katika hospital yetu.

Huduma ya kiroho 

Huduma ya kiroho ni kitu cha msingi sana hapa hospitlini kwetu, kwa heshima ya kila imani, kikanisa kidogo cha hapa hutumika kutoa huduma ya misa, na masakramenti.
Ushauri wa kiroho hutolewa na jumuiya ya mapadre waliopo hapa, mashirika ya masista wanaofanya kazi hapa na makatekista. Viongozi wa Kiroho wa madhehebu mengine wanaalikwa kuja kutoa huduma wakihitajika.