UTAYARI WA KUFANYA KAZI KWA KUSHIRIKIANA HUSAIDIA IDARA.

HUDUMA

NA MADAWA

HUDUMA NA MADAWA

Hospitali ni kama “mashine” kubwa. Hufanya kazi tu kama vyuma vyote huungana katika utume mmoja: kwa sababu hii, katika hospitali yetu hakuna tu idara 6 kubwa lakini pia ina idara nyingine za miundo mbinu ambazo huwezesha utekelezaji wa shughuli zote za hospitali.
h

Maabara

Maabara hushghulikia vipimo vya wagonjwa kimaabara kwa wagonjwa kwika idara zote 6. Maabara hupokea sampuli na kutoa majibu ya vipimo katika saa zote 24 za siku. Hii husaidia madaktari kufanya matibabu sahihi na kwa haraka.

Huduma nyinginezo za matibabu

Matibabu kwa njia ya mazoezi

Matibabu haya ni muhimu kwa mazoezi ya viungo kwa wagonjwa wengi baada ya matibabu ya upasuaji au ya dawa. Ni muhimu sana kwa watoto waliozaliwa na vilema, ya kuungua moto au majeraha mbali mbali.
k

Famasia

Famasia ni eneo ambapo madawa mbalimbali hutunzwa na kusambazwa katika idara tofauti. Katika famasia kuna wanataaluma na wasaidizi wanaotoa huduma kulingana na mahitaji.

Magonjwa ya meno

Chumba kwa ajili ya meno katika hospitali kinatoa huduma kila siku hata huduma za dharura. Wengi wa wagonjwa wanaofika katika idara ya meno wanakuwa na magonjwa ya kuambukiza katika meno au fizi. Wengi huja kwa kuchelewa na kwa hiyo meno yao yanang’olewa.

X-Ray na Ultrasound

Uchunguzi kwa njia ya x-ray au ultrasound husaidia sana katika uchunguzi wa magonjwa yanayohitaji picha kabla ya upasuaji au matibabu mengine. Mara nyingi ni muhimu sana kupata picha kabla ya kufanya upasuaji uliopangwa au wa dharura.

Magonjwa ya macho

Huduma ni ya muhimu na mara nyingi watu wanaoishi vijijini hawaipati, kwani bado haijapewa kipaumbele kikubwa. Katika kitengo cha macho wagonjwa hutibiwa maradhi mbali mbali ya macho na kupimwa uoni.

Uchangiaji wa Damu salama

Tukishawishika kwamba utamaduni wa zawadi hauna mipaka pia katika hospitali yetu tangu mwanzo kabisa tumeendeleza huduma ya uchangiaji damu ikiwa inashangaza kwa kuwa na wachangiaji wengi wanaojitolea.

Huduma ya madawa

Kitua cha unyweshaji dawa

Moja kati ya habari za hivi karibuni katika hospitali ya mtakatifu Gaspari ni mafanikIo ya kutengeneza maji hayo hapa hospitalini badala ya kuyaagiza kutoka mbali. Kimsingi kitengo hiki kinajihusisha kutengeneza aina mbalimbali za maji ya “drip” karibu chupa 30,000 kwa mwaka
]

Mochwari

Mochwari mpya ilifunguliwa 2018, kwa sasa ina vyumba vya ubaridi na meza kwa ajili ya kufanyia uchunguzi. Huduma hii inaruhusu maiti kuhifadhiwa kwa muda mrefu mpaka hapo familia itakapochukua mwili huo.

Maji salama ya kunywa

Tangu mwanzo wa utume katika nchi ya Tanzania ilikuwa tamaa ya wamisionari kuwapatia wagonjwa na wakazi wa eneo hili maji yaliyochujwa. Maji hayo kwa kiwango kikubwa yamepunguza maambukizi ya magonjwa mbalimbali ya matumbo.

Jiko

Wagonjwa, ndugu, na wanaowatunza wana uwezo wa kujipikia chakula wawapo hospitalini, japo pia hospitali hutoa huduma ya chakula kwa maskini na wasio na waangalizi.

Chumba cha watoto na cha michezo

Kwa mtazamo kwamba mazingira ya hospitali huleta mwelekeo wa msongo wa mawazo hasa kwa watoto, iliamuliwa kutengeneza chumba chenye kumfanya mtoto aburudike na kucheza akiwa hospitalini.

TIMU KUBWA YENYE UTUME MMOJA!

Madaktari, wataalamu wengi na wafanyakazi wanahakikisha mazingira yanakuwa safi, kuendeleza ukarabati na umakini wa nyaraka.

MIRADI

WAAJIRIWA

WAGONJWA kila mwaka

VIPIMO VYA MAABARA kwa mwaka

HUDUMA KWA WATANZANIA

Utume wa hospitali ya Rufaa ya Mtakatifu Gaspari na Chuo cha Mafunzo ya Uuguzi unaeleweka kwa wote, watumishi wageni na wazalendo, kama utume wa kutoa huduma kwa watanzania unaoongozwa na haki ya kujali utu wa kila mtu.

WATU WENGI WENYE DHUMUNI MOJA

Katika hospitali ya Mtakatifu Gaspari tuna dhumuni moja: kutoa huduma bora kwa wote wanaohitaji. “tunapaswa kufanya mengi kwa haraka na vizuri” alisema Mtakatifu Gaspari

“Lazima tufanye mengi, vizuri na haraka”

Mt. Gaspari del Bufalo 

una maswali yoyote au unataka habari? Andika sisi!Andika sisi!

St. Gaspar Hospital

P.O. BOX 12, Itigi – Singida – TANZANIA

Fax: +255 732 -960 744

Nambari za simu:

+255 755454040
+255 26 254 0193

E-mail:  

info@stgasparhospital.org

Hospitali

– Tovuti rasmi

Hospitali leo

Huduma maalum

Booking

Tusaidia

 

 

 

Link utili

Sera ya afya

Wamisionari wa Damu Azizi General Curia

Wamisionari wa Damu Azizi – Tanzania

– Wamisionari wa Damu Azizi – Italia