Utume wetu

Hospitali ya Rufaa ya Mtakatifu Gaspari inapaswa kuwahudumia watu walio pembezoni mwa jamii kwa kuwapatia huduma za kitabibu, elimu juu ya kujikinga na magonjwa mbali mbali; vyote hivi vikijikita katika misingi na kanuni za kikristo. Huo ni utume wetu. Hospitali yetu inataka kuwa kiini cha maelekezo mazuri ya huduma za kiafya.
Waganga wa Hospitali ya Mtakatifu Gaspari hutumia vifaa tiba vizuri na vya kisayansi kwa usahihi na ukamilifu. Dhumuni letu ni kuhudumia na kukuza utu kiroho na kimwili. Hospistali ya Mtakatifu Gaspari inastawisha mazingira bora, uponyaji, faraja, elimu, heshima na uwazi. Tunathamini ubunifu, ugunduzi, fikra pevu na kuweka katika matendo fikra mpya za matabibu. Kwa sababu hiyo tunathamini na kuinua uwezo wa madaktari na wafanyakazi mbalimbali.

I

Uponyaji

Mtu anayekuja Itigi anafahamu kwamba anaweza kufaidika na utaalamu huo wa kitabibu.
I

Faraja

Utume wetu unaweka kipaumbele kuwajali ndugu zetu katika machungu na maumivu yao.
I

Uelimishaji

Hapa Itigi kuelimisha kunamaanisha kuweka matumaini katika maisha yajayo kwa kutoa utaalamu wetu kwa kila mmoja.
\

Kanuni

Kadiri ya mafundisho ya kikristo, tunaamini kabisa kwamba kila mmoja ana utu na haki ya kupata huduma. Ndani ya hospitali yetu maisha ya kila mmoja yanathaminiwa na kutunzwa kwa ukarimu.

\

Utume

Tunahitaji kuwahudumia watu waliopo pembezoni na wote wanaohitaji msaada wa matibabu. Tunahitaji kutoa huduma bora za kitabibu.

\

Watumishi

Bendera ya hospitali yetu ni watumishi. Waajiriwa wetu hufanya utume wetu kuwa wao, huishi kikamilfu katika falsa hii ya utume.

mahali

St. Gaspar Referral Hospital

P.O. 12 – Itigi (Singida)

 

email

info@stgasparhospital.org

nambari ya simu

(+255) 262540193

(+255) 755454040

St. Gaspar Hospital

P.O. BOX 12, Itigi – Singida – TANZANIA

Fax: +255 732 -960 744

Nambari za simu:

+255 755454040
+255 26 254 0193

E-mail:  

info@stgasparhospital.org

Hospitali

– Tovuti rasmi

Hospitali leo

Huduma maalum

Booking

Tusaidia

 

 

 

Link utili

Sera ya afya

Wamisionari wa Damu Azizi General Curia

Wamisionari wa Damu Azizi – Tanzania

– Wamisionari wa Damu Azizi – Italia