CHUMBA CHA DHARURA

 

 

IDARA YA WAGONJWA

WA NJE

MASAA 24 YA DHARURA NA HUDUMA YA CLINIKI

MAPOKEZI YA MGONJWA

Mara mgonjwa anapoingia hospitali, anapokelewa na wauguzi wawili ambao hufuata itifaki maalum- wanatathmini hali ya mgonjwa,wanakuchukua na kurekodi vipimo vya msingi. Wakitambua mgonjwa anayehitaji matibabu ya haraka wanampeleka hima kwa daktari.

UCHUNGUZI WA KITABIBU

Baada ya triage mgonjwa asiyehitaji huduma ya dharura anapelekwa kufunguliwa jalida na anapelekwa kwa daktari kwa uchunguzi na vipimo.

 Katika IDARA YA OPD kuna vyumba vitatu vya uchunguzi wa awali na matibabu. Kila chumba kina daktari ambaye huona wagonjwa na kuagiza vipimo vya awali kufanyika. Sampuli za vipimo huchukuliwa na kupelekwa maabara.

Kwa namna hii muda wa kusubiri unaweza kupunguzwa kwa kiwango kikubwa.

 

MATIBABU 

Baada ya uchunguzi wa kitabibu na kupata matokeo ya vipimo vya awali, daktari anaweza kuamua kumtibu na kukamilisha matibabu ya mgonjwa pale OPD, au akampeleka katika kliniki ya dakatri bingwa kwa uchunguzi zaidi. Aidha anaweza kumlaza wodini mgonjwa liyezidiwa moja kwa moja kutokea OPD.

 Mwaka 2018 wagonjwa 6178 (19%) kati ya wagonjwa 31450  waliopitia OPD ndio waliolazwa.

 

MAGONJWA MAKUBWA MATANO KATIKA MAHUDHURIO YA OPD

%

MAAMBUKIZI

%

MAJERAHA (AJALI, KUUNGUA...)

%

YA MALARIA

%

KIKOHOZI NA KICHOMI

%

MAGONJWA YA MATUMBO

VIONGOZI WA IDARA

Supervisors: dr.  Hilda makule peter – nz. SR. DELPHINA RAPHAEL TEMU

MADAKTARI WETU 

Kuna madaktari wanane ambao hupokezana zamu pale OPD. Madaktari hawa wanao uwezo wa kumudu magonjwa yote ya kawaida. Pia wana uwezo wa kuanzisha matibabu ya dharura kwa wagonjwa waliozidiwa. Hupeana zamu katika kutoa elimu kwa uma unaofika OPD kuhusu magonjwa mbali mbali na namna ya kujikinga nayo.

Wengi wa madaktari hawa ni vijana walio na uwezo wa kujifunza haraka.

ZAIDI ya 30000

wagonjwa HUINGIA OPD KILA MWAKA

WAUGUZI WETU

Katika OPD yetu tuna wauguzi 18 na wasaidizi wengine. Wote waathamini kazi yao ya kuhudumia wagonjwa wanaofika kutibiwa. Wanatenda kazi zao kwa umakini, kwa haraka  na kwa kujituma.

 

 

 

Zaidi ya 6178

WAGONJWA HULAZWA KUPITIA OPD

WAFANYAKAZI MADAKTARI WETU

OPD ni kama hospitali ya ndani ya nyingine: msaada wa haraka, huduma makini,  kwa namba kubwa ya wagonjwa. Kwa sababu hii, kando ya matibabu yetu na mzunguko wa wauguzi, muundo wetu pia una wasaidizi watano ambao hudhamini usafi, na wengine watano walioajiriwa huwahudumia wagonjwa kwa kuwasajili, mzunguko wao kwenye wodi na Nyanja ya kiuchumi.

zaidi ya 80

WAGONJWA 80 KWA SIKU

St. Gaspar Hospital

P.O. BOX 12, Itigi – Singida – TANZANIA

Fax: +255 732 -960 744

Nambari za simu:

+255 755454040
+255 26 254 0193

E-mail:  

info@stgasparhospital.org

Hospitali

– Tovuti rasmi

Hospitali leo

Huduma maalum

Booking

Tusaidia

 

 

 

Link utili

Sera ya afya

Wamisionari wa Damu Azizi General Curia

Wamisionari wa Damu Azizi – Tanzania

– Wamisionari wa Damu Azizi – Italia