wodi
ya uzazi
Wakuu wa wodi
Dr. Simon Mrema – Nz. Aurea Macha
vitanda
wataalamu
WATOTO HUZALIWA
idara yetu
Wodi ya uzazi imejikita katika maswala ya uzazi na magonjwa ya kike, na ina uwezo wa kutoa huduma kwa mama na mtoto anapokuja hospitalini kwa matatizo ya uja uzito au kujifungua. Wodi ina jumla ya vitanda vya kawaida 36.
Sehemu ya kujifungulia ina vitanda vinne vya kuangalia mwenendo wa uchungu na vitanda viwili vya kujifungulia. Vitanda vingine vinane ni kwa ajili ya magonjwa ya kike mbali na uzazi.
Madaktari mara nyingi hujikuta wakitoa huduma tofauti tofauti au za dharura zinazoendana na hali ya uja uzito kama vile kifafa cha mimba, maambukizi (sepsis) uzazi pingamizi,upungufu mkubwa wa damu na matumizi ya dawa za asili.
Kwa zaidi ya miaka 30 wodi ya uzazi imekuwa wodi kimkakati katika hospitali yetu. Vifo vya kina mama na watoto vimepungua kwa kwa asilimia 80 katika miaka mitano iliyopita.
Maendeleo mengi yamefanyika, japo bado kuna mahitaji makubwa ya maboresho.
habari mpya
Vyeti vya NACTE vimetoka
Kwa wahitimu wa stashahada ya miaka mitata...
Usajili uko wazi kwa mwaka mpya wa shule Mt. Gaspari
Usajili uko wazi kwa mwaka mpya wa shule katika...
TANZAGO – Chuo cha Uuguzu cha Mt. Gaspari
TANZAGO Kutokana na tangazo lililotolewa na...